Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Prof. Said Mohamed, ametangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) na mitihani ya ualimu iliyofanyika Mei mwaka huu.
Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar es Salaam amesema matumizi ya programu ya ChatGPT katika kufanya udanganyifu yameibuka kwa mara ya kwanza kwenye mitihani ya taifa kwa wanafunzi wa kidato cha sita.
Imeelezwa kuwa kuna baadhi ya watahiniwa wamekamatwa na simu wakitumia ChatGPT kutafuta majibu, wengine walibainika kuingia na vikaratasi kwenye vyumba vya mitihani.
© 2026 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED