Kocha wa Misri, Hossam Hassan, amesema timu yake ‘imeibiwa’ nafasi ya kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia 2026 baada ya kufungwa mabao 3-2 na Argentina katika mchezo uliogubikwa na utata wa uamuzi wa waamuzi wa VAR.
Misri ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 kabla ya Argentina kutoka nyuma na kupata ushindi uliwawezesha kutinga robo fainali, lakini Hassan anaamini matokeo hayo yaliathiriwa na uamuzi usio na haki.
"Sihitaji kuzungumza kuhusu bahati mbaya. Leo (jana) tumeibiwa waziwazi na tumetendewa dhuluma," alisema Hassan baada ya mchezo.
Utata ulianza kipindi cha kwanza baada ya bao la Mostafa Zico kufutwa kufuatia VAR kubaini kuwa kulikuwa na faulo dhidi ya Lisandro Martínez mwanzoni mwa shambulizi hilo.
Hata hivyo, Zico baadaye alifunga tena na kuipa Misri bao la pili, jambo lililoifanya timu hiyo kuwa karibu sana kufuzu kwa mara ya kwanza katika historia yake kwenda robo fainali ya Kombe la Dunia.
"Hatujaoneshwa heshima wala haki. Penalti yetu haikutolewa na hata VAR haikuangalia tukio hilo. Pia tuliona bao letu likifutwa kwa namna ya kushangaza," alisema kocha huyo.
Hassan aliongeza kuwa amepoteza imani na mwenendo wa mashindano hayo kiasi hataendelea kuyafuatilia.
ESPN
© 2026 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED