Wananchi wapatiwa uelewa kuhusu gesi

By Elizabeth Zaya , Nipashe Jumapili
Published at 03:59 PM Jul 05 2026
Wananchi wapatiwa  uelewa kuhusu gesi
Picha: Elzabeth Zaya
Wananchi wapatiwa uelewa kuhusu gesi

BAADHI ya wananchi wamesema elimu wanayoipata kuhusu matumizi ya gesi asilia imewapa uelewa mpana wa namna ya kutofautisha kati ya gesi inayotumika kwenye magari na inayotumika kwa ajili ya kupikia.

Wakizungumza katika  banda la Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA),  kwenye  Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu Sabasab, waliofika kupatiwa elimu hiyo, wamesema kwa sasa wameelewa tofauti Kati ya gesi asilia na gesi ya mitungi (LPG) inayotumika kupikia.

Wameeleza kuwa kupitia elimu hiyo pia wameelewa namna ya kutofautisha majukumu yanayofanywa na PURA, EWURA, pamoja na TPDC. 

PURA inaendelea kushiriki na kutoa elimu kwa wananchi  katika maonesho hayo.