‘Matumizi makopo, ndoo, visado hayatakiwi kwenye biashara’

By Ida Mushi , Nipashe Jumapili
Published at 04:10 PM Jun 14 2026
Bidhaa katika ndoo tayari kwa kuuzwa
Picha: Idda Mushi
Bidhaa katika ndoo tayari kwa kuuzwa

WAKALA wa Vipimo Mkoa wa Morogoro umewataka wafanyabiashara kuzingatia matumizi ya vipimo vilivyoidhinishwa na kuachana na makopo, ndoo za plastiki na visado, ambavyo havitambuliki kisheria katika upimaji wa bidhaa.

Meneja wa Wakala huo mkoani Morogoro, Deogratias Hussein, anatoa rai hiyo wakati wa kugawa mizani kwa wafanyabiashara wa Soko la Mboga, Feri Magole wilayani Kilosa.

Amesema matumizi ya vipimo visivyo rasmi yanaweza kusababisha udanganyifu na kuathiri haki za walaji pamoja na wafanyabiashara wenyewe, hivyo mamlaka yake itaendelea mamia utekelezaji wa sheria za vipimo.

Mizani
Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Vipimo Tanzania, Francis Olwero, amesema taasisi hiyo inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa kutumia vipimo vinavyokubalika kisheria.

Mwenyekiti wa Soko la Mboga Feri Magole, Mohamed Said, amesema kuwa ugawaji wa mizani unaongeza uwazi katika biashara na kusaidia kuondoa changamoto za vipimo visivyo rasmi.