Rais wa Kenya, William Ruto, yupo mjini Baku, Azerbaijan kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa upanuzi wa miji (World Urban Forum), akitarajiwa kuonesha mpango wake wa ujenzi wa makazi ya bei nafuu kama mojawapo ya njia za kukabiliana na uhaba wa makazi duniani.
Mpango huo wa ujenzi wa makazi ya bei nafuu, aliuanzisha pindi tu alipochaguliwa 2022, ingawa ulipingwa mahakamani na baadhi ya wakenya ambao walihisi kuwatoza wafanyakazi kodi ya asilimia 1.5 ya mshahara kufadhili mradi huo ilikuwa kinyume cha sheria.
Mahakama ilisimamisha mpango huo kwa muda kabla ya bunge kupitisha muswada wa serikali na kuifanya kuwa sheria kwa wafanyakazi kulipa kodi ya makazi almaarufu (Affordable Housing levy).
Kwa mujibu wa Wizara ya Ujenzi na Nyumba, Idara inayosimamia mpango wa ujenzi wa makazi ya bei nafuu imerekodi kwamba nyumba 111,975 zimekamilishwa katika kaunti 47 nchini Kenya, huku wanunuzi wakijiandikisha katika mpango wa Boma Yangu na kulipa pole pole kwa kipindi cha miaka 30.
Katika kikao cha makazi kinachoandaliwa nchini Azerbaijan kati ya May 17 na 22, Kenya inajiandaa kuonesha jinsi serikali za mataifa mengi duniani zinavyoweza kutumia ufadhili wa ndani kukabiliana na uhaba wa makazi. 
Mkutano wa kwanza wa makazi wa kimataifa uliandaliwa Kenya mnamo 2002.
Chanzo: BBC
© 2026 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED