NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amesema serikali imehakikisha kuna mazingira tulivu ya uwekezaji, kwa kuweka masharti ya kikodi ambayo ni rafiki, huku ikiondoa kanuni zilizokuwa kikwazo zaidi 370.
Londo amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati utambuzi wa kampuni bora 100 za chapa za Afrika zinazotengeneza bidhaa zilizoko barani humo, jijini Dar es Salaam.
Amesema kwamba pia bajeti ya fedha kwa mwaka 2026/2027 imekuwa ya kwanza katika kuanza utekelezaji Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku kwa asilimia 70 ikitegemea utendaji kazi wa sekta binafsi.
“Tunatambua mchango wa sekta binafsi, watoa huduma na serikali inaunga mkono juhudu hizo za watanzania na wanakuwa washiriki wa kweli katika mnyororo wa thamani,” amesema.

“Mwaka wa nne tunawatambua wazalishaji hao sasa, watu walioshiriki kuwania ni takribani 5,000 hadi kufikia mchakato wa kampuni 500, kutoka katika nchi zaidi ya saba,” amesema Kilawe.
© 2026 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED